Njia rahisi ya kutengeneza scones

Image result for Scones
Aina mojawapo ya scones

Scones zipo za aina nyingi lakini utengenezaji wake huwa ni rahisi tu. Hapa nitakupa moja ya mbinu za kutenengeneza moja wapo ya scones.
Mahitaji


  • Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
  • Sukari (sugar 1/2 kijiko cha chakula)
  • Chumvi (salt 1/2 kijiko cha chai)
  • Hamira (yeast 1/2 kijiko cha chakula)
  • Baking powder 1/2 kijiko cha chai
  • Siagi (butter 1/4 ya kikombe cha chai)
  • Maziwa (fresh milk 3/4 ya kikombe cha chai)(unaweza kutumia maji badala ya maziwa)
Matayarisho
Pasha maziwa yawe ya uvuguvugu kisha weka pembeni, pia yeyusha siagi na uweke pembeni.
Baada ya hapo tia kila kitu kwenye bakuli la kukandia kasoro maziwa, na uchanganye vizuri.
 tia maziwa kidogo kidogo katika mchanganyiko huo kisha  ukande. Ukimaliza uweke kwenye sehemu ya joto na uache uumuke. Ukisha umuka utawanyishe katika madonge saba Kisha .pakaza mafuta au siagi katika chombo cha kuokea kisha yapange  hayo madonge katika hicho chombo na uyaache yaumuke tena . Baada ya hapo pakaza mafuta juu ya hayo madonge na uyaoke  katika oven kwa muda wa dakika 25 na hapo scones zitakuwa tayari

Comments

Popular Posts