Jifunze jinsi ya kuandaa burger ya nyama ya ng'ombe

Utakachohitaji ni:


  • Nyama ya kusaga
  • Tango
  • Unga wa mkate
  • Kitunguu swaum kilichosagwa
  • Kitunguu maji
  • Tangawizi iliyosagwa
  • Nyanya
  • Yai moja
  • Lettice
  • Chumvi
  • Mayonnaise
  •  mikate ya burger 3
  • ketchup.
Baada ya kuwa na vyote hivyo sasa fanya yafuatayo:

Tia minofu ya nyama ya ngo'ombe kwenye bakuli kisha weka  chumvi, unga wa mkate, yai, kitunguu swaum,tangawizi na  kitunguu maji  na kisha uichanganye vizuri na uitawanyishe katika madonge 3 Baada ya hapo iache ikae kwa muda wa dakika 30 na itakuwa tayari kwa kupikwa.  Pika upande mmoja mpaka uive na kisha ugeuze upande wa pili na pia uupike mpaka uive katika moto mdogo.
Image result for Beef burger
Beef Burger
Ikiwa hauna jiko la mkaa unaweza kutia kwenye oven na uiache kwa muda wa dakika 15 au 14ukiigeuza kila upande kwa kitambo mpaka itakapoiva.
Baada ya hapo andaa mkate wa burger kwa kuukata kati kisha katakata tango, kitunguu,nyanya na lettice.Kisha anza kuvipanga kwenye mkate wa burger kwa kuweka lettice chini kisha tango,nyanya, vitunguu na kisha burger yenyewe. Baada ya hapo tia mayonnaise na ketchup juu ya burger na upange tena vitunguu, nyanya, tango na lettice. Baada ya hapo weka mkate wa burger kwa juu na burger itakuwa tayari kwa kuliwa.
 

Comments

Popular Posts